Genesis 34:2-6

2 aIkawa Shekemu mwana wa Hamori Mhivi, mtawala wa eneo lile alipomwona, akamchukua na kumnajisi. 3Moyo wake ukavutwa sana kwa Dina binti Yakobo, akampenda huyu msichana na akazungumza naye kwa kumbembeleza. 4 bShekemu akamwambia baba yake Hamori, “Nipatie msichana huyu awe mke wangu.”

5 cYakobo aliposikia kwamba binti yake Dina amenajisiwa, wanawe walikuwa mashambani wakichunga mifugo yake, kwa hiyo akalinyamazia jambo hilo mpaka waliporudi nyumbani.

6 dKisha Hamori baba yake Shekemu akaenda kuzungumza na Yakobo.
Copyright information for SwhNEN